Masai ya wanawake - Page 2



Kwa mujibu wa utafiti uliowahi kufanywa na gazeti hili la Mwananchi miaka minane iliyopita wilayani Loliondo, Wamasai wana upendo wa kimila uliopitiliza ambao hauwezi kuonekana kwa makabila mengine kwa sababu hufanyika katika mazingira ya siri ili kuzuia usumbufu na kero.
Upendo huo ni ule wa kupeana watoto. Wanawake ambao kwa bahati mbaya hawajabahatika kupata watoto hawafukuzwi kama inavyofanyika kwa makabila mengine bali hupewa watoto kwa siri makusudi kuepusha fadhaa na adha ya ugumba, tatizo ambalo husumbua ndoa nyingi.
Siri hii ni kubwa miongoni mwa jamii yao na wanawake wanaotoa watoto wao kuwapa ndugu au rafiki zao, hutakiwa kuitunza.
Laibon (mganga wa jadi) wa jamii ya Wamasai wa Wasso, Mkenga Kitupey, aliliambia gazeti hili kuwa wakati wa makabidhiano ya mtoto, mwanamke ambaye hajazaa hutakiwa kumpa aliyezaa ndama jike.
Mkenga alisema ndama huyo hufanyiwa dawa za kimila kama maagano kati ya wanawake hao wawili. Agano kuu ambalo wanawake hao huwekeana ni kutunza siri.
Mtoto wa Kimasai anapozaliwa hapewi jina rasmi, bali hupewa jina la muda lijulikanalo kama ‘embolet’, ikiwa na maana ya kufungua.
Kuanzia siku ya kuzaliwa, hadi siku ya sherehe ya kumtaja mtoto, atatambuliwa kwa jina la embolet. Watoto wa Kimasai hutofautiana kiumri wakati sherehe ya kuwapa majina inapofanyika.
Kulingana na nasaba ya familia zao, baadhi yao wanaweza kuwa na umri wa miaka mitatu kabla ya kufanyika kwa sherehe ya majina ya watoto wa Kimasai, inayojulikana kama ‘Enkipukonoto Eji’ ikimaanisha kutoka kifungoni au kutoka katika hali ya kutengwa. Katika maandalizi ya sherehe za Enkipukonoto Eaji, mama na mtoto hukaa tu ndani na kuacha nywele zikue zaidi.
Maandalizi ya sherehe za majina ya watoto wa Kimasai huchukua hadi siku mbili na huhusisha shughuli mbalimbali.
Ni wanawake pekee wanaoruhusiwa kula nyama ya kondoo huyo.




